Tuesday, November 23, 2010
WAKUSWAMPA KITAA
Usifikirie sherehe bali alikwenda kusutwa mtu na matarumbeta,kwa bahati mbaya hawakumkuta hikabidi wamsubili mpaka arudi kazini.
Monday, November 8, 2010
WAKUSWAMPA KITAA
Friday, November 5, 2010
WAKUSWAMPA KITAA
Hapo juu ni picha za Tukio lililotokea usiku wa kama saa 2 hivi jana baada ya wasimamizi wa uchaguzi katika kata ya Kiwalani kuondoka na askari wakiwa ktk magari ya polisi na masanduku ya KURA kabla ya kutoa matokeo hasa ya Udiwani ambayo watu wengi walikuwa wakuyasubiri kwa hamu..
Huku nyuma watu wakaona wamefanywa wajinga, kwa hasira wakachoma moto ofisi hizo! Laiti matokeo husika yangetolewa mapema ofisi isingechomwa moto
Bi kidude
Hellow evrybady!
ningependa kuwataarifu kwamba mwanamuziki wenu kipenzi Diamond nimechaguliwa katika tunzo za MTV BASE MAMA'S AFRICA kuwania tunzo ya BEST NEW ACT..tafadhari ukiwa kama fan wangu,ndugu yangu, au rafiki yangu kipenzi naomba unipigie kura kupitia site hiyo hapo chini ili... niweze kushinda tunzo hii na kuufanya mziki wetu uzidi kutambulika ulimwenguni...
akhsante!
http://www.mama.mtvbase.com/nominees.html
Tuesday, November 2, 2010
ANT EZEKIEL
Nina sababu nyingi za kumuelezea huyu msanii,moja ya sababu hizo ni kwenye movie mpya iliyotoka hivi karibun inayoitwa SIGNATURE kwa kweli amejua kuuvaa uhusika wa kile alichokuwa anafanya,bira ya ubishi tafuta film hii kisha itazame bira ya usumbufu hapo utaona kweli dada huyu hauzi sura kwenye film bali anatafuta chapaa.
KEVIN HATUA BONGO
Mshindi wa Big brother revolution mwaka jana KEVIN CHUWANG akiwa na familia yake ametua hapa bongo kwa ajili ya kutoa mahali ya dada yetu Elizabeth tayari kwa maandalizi ya harusi yao itakayofanyika mwezi wa pili mwakani.Katika moja ya vikao vyake hapa Dar Kevin aliniita ili kushauriana mambo kadha wa kadha juu ya harusi yao lakini pia juu ya project zake anazotarajia kufanya Africa mashariki.Binafsi nilianza kujuana na Kevin katika jumba la big brother revolution mwaka jana ambapo mimi nilikuwa humo kama star mwalikwa tu,wakati naondoka katika jumba hilo baadhi ya housemate kama Hannington,Leonel nk waliniomba nguo zangu lakini Kevin yeye aliomba nimpatie jina la The great,nami nilimwita Kevin The great nikimwambia kuwa atakuwa the great wa jumba hilo,hatimae alishinda na kuzidi kuwasiliana nami.
PWEZA PAUL AFARIKI
PWEZA aitwaye Paul aliyejizolea umaarufu wakati wa michuano ya kombe la Dunia Afrika Kusini 2010 kwa kutabiri matokeo kwa uhakika, amekufa jana asubuhi na kuelezwa kuwa amekufa kifo cha kawaida.
Wakati wa mashindano ya Dombe la Dunia alikuwa akitimiwa kwa utabiri kwa kumwekea mkebe ulikuwa na chakula chake na bendera za nchi ambapo, mahali alipoenda ndipo ilipewa nafasi na kushinda, na ilikuwa hivyo.
Pweza huyo alikufa akiwa katika katika kituo cha Oberhause, Ujerumani ambapo alikuwa akihifadhiwa. Kifo cha pweza huyo kimewasikitisha mashabiki wa soka wa Ujerumani na sehemu mbalimbali duniani.
"Tumesikitishwa kwa kujua kuwa alifurahia maisha mzuri hapa," alisema Stefan Porwoll, meneja wa kituo cha Oberhausen Sea Life Center kilichopo magharibi mwa Ujerumani. Alikuwa akikuwa akikua kawaida na tutamkosa sana."
"Paul aliishangaza dunia kwa kutabiri kwa usahihi wakati wa mapambano ya Ujerumani na kisha kutabiri fainalil," Porwoll alisema,kwa mujibu wa CNN.
Kituo hicho kinapanga taratibu za mazishi.
Subscribe to:
Posts (Atom)